Anti Ahmadiyya Movement in Islam
12th December 2003

BISMILLAHIR RAHMANIR RAHIIM

Kwa nini niliachana na uahmadiyya?

[mahususi kwa waahmadiyya,lakini pia waislamu wanaweza kusoma]

[Na profesa Munawwar Ahmad Malik]

Profesa Munawwar Ahmad Malik alikuwa ni kadiyyani kwa takriban miaka 40. mnamo mwak 1999 Allah akamuongoa na akafungua moyo wake akakubali uislamu.na kuutupilia mbali ukadiyyani.hivi sasa Profesa Munawwar anafanya kazi ya kufichua hadharani siri za dini hii ya ukadiyyani ili wafuasi wagutuke na kuona mambo yanayofichwa.

Rafiki zangu wapendwa wanajumuiya!

Nataka kuzungumza nanyi mambo kadhaa muyasikilize kwa makini mambo hayo ambayo yanatakiwa kutafakariwa na kufanyiwa uchunguzi. Kwa vile mimi nimeishi katika jumuiyya hii kwa miaka 40 bila shaka hamuwezi kuyapinga mambo hayo nitakayosema.wakati nikiwa ahmadiyya mkereketwa nimeshiriki katika tabligh kama mubaligh na kama mwanaharakati wa kawaida nimeshiriki kikamilifu katika kila shughuli za jumuiyya. Hatimayue nikawa naibu Amir wa jumuiyya ya Jhelun na baada ya kushirikiana na viongozi wa juu wa jumuiyya na kuona nyendo zao nikatafakari na kufanya uchunguzi wangu hapo ndipo Allah aliponipa muongozo wake.nikaachana na jumuiyya hii na kuingia katika uislamu. Kama mtathubutu kuyapinga yale nitakayosema kwamba si ya kweli basi mimi nitakuwa na haki kusema kwa hakika hamjui undani wa jumuiya hii au kwa sababu mnalipwa pesa kama murrabi.

Enyi rafiki zangu wapendwa!

Ninyi mwajua kwamba tokea utotoni akili ya kila mtoto wa kiahmadiyya inapandikizwa imani hii kuwa uahmadiyya ni uislamu halisi kwamba katika zama hizi Mungu ameipa Ahmadiyya jukumu la kushika hatamu kamili za uislamu kwamba uislamu wa waislamu wengine umeharibiwa na kugeuzwageuzwa kwamba Ahmadiyya ndiyo inawakilisha ule uislamu uliokuwepo enzi zile ulipoanza.

Wapendwa rafiki zangu katika jumuiyya!

Nguzo za uislamu ni tano ambazo kila mfuasi wa jumuiyya anazikubali nazo ni Shahada mbili, Sala, Zaka, funga na hijja hizo ndizo nguzo pekee za uislamu na hapana kukubali kuwa nguzo hizi hazitimilizi matakwa ya uislamu

Wapendwa rafiki zangu katika jumuiyya!

Kuna msisitizo mkubwa wa kutoa michango katika jumuiya chanda Aam ndio mchango mkubwa unaotolewa na kila mtu mwenye kipato [na sasa umekuwa lazima hata kwa watu wasio na ajira nao pia watoe] mchango huu ni wa lazima na kila mtu mwenye ajira lazima atoe asilimia 6.25 ya mshahara wake unapindukia mwaka wanajumuiyya wote wanatakiwa kuzingatia hilo.

Mara mbili au tatu kila mwaka wakaguzi huakikisha kuwa makusanyo ya michango yanafikiwa asilimia 100% Ili kutia msukumo katika ukusanyaji motisha utolewa. Wale watakaofikisha asilimia 100%majina yao yatapelekwa kwa kwa huzoor [mirza Tahir Ahmad Qadian sasa ni hayati kwa sasa hupelekwa kwa Mirza Tahir [sasa ameshafariki badala yake ni Masroor] kwa ajili ya kuombewa dua na nyakati fulani fulani majina yao yatakuwa yanatajwatajwa n.k

Kabla ya mwisho wa mwaka wa fedha viongozi wa jumuiyya hutoa hotuba juu ya umuhimu wa chanda [mchango] na kusisitiza ukusanyaji wake na mwishoni mwa mwaka maelezo ya mchango huo hutolewa, ahadi za michango hutolewa na bajeti ya mwaka unaofuata hutangazwa.

Kwa kila mtu awe na kazi asiwe na kazi mchango wa tahreek jadeeed ni lazima.kuweza kufikia 100%ya makusanyo ya chanda tahreek jaded wakaguzi mbalimbali hutawanywa kutoka kituo kikuu, viongozi hutoa hotuba na chombo kizima cha jumuiya hushughulika na ukusanyaji wa mchango huu.

Mchango wa "chanda salana" nao lazima kila mwaka kima cha mchango huu ni asilimia 10%ya kipato cha mwezi kusisitiza makusanyo yake hotuba maalum hutolewa.nayo chanda ya ‘wakf jadeed’ pia ikaanzishwa ambapo mwanzoni ulikuwa mchango wa hiari lakini hivi sasa ni mchango wa lazima. Wakaguzi waliotajwa katika aina zote NNE za michango huja kutoka kituoni mara tatu kila mwaka kufuatilia makusanyo ya michango hii [chanda] wakaguzi hufika hata majumbani kukusanya michangokwa wanaotakiwa kutoa michango hiyo.

Mbali ya hii kuna michango mingine [chandas]

Mathalani Kwa vijana [khudamul-ul-ahamadiyya] kuna michango ya majlis, ta’amer hall, ijtma’a Kwa watu wazima [Ansarullah] kuna mchango wa Bosnia, Afrika n.k chanda ya miaka100 ya jubelee ilikusnywa Kwa miaka 16

Mfuasi wa Ahmadiya ambaye mshahara wake ni Rs 3000 kwa mwezi anatakiwa kutoa angalau Rs 300 kwa mwezi katika michango hii kama mke,watoto na wazazi wako pamoja naye basi nao sehemu ya michango yao itatoka katika mshahara huohuo hivyo mtu huyu hutakiwa kutoa kati ya Rs3000 hadi500 kila mwezi.na asipolipa atalimbikiziwa katika hesabu yake ambapo mwisho wa mwaka atalazimika kulipa kati ya Rs3000 hadi4000 vilevile kama mtu anakipato cha Rs10,000 kwa mwezi basi ni lazima alipe zaidi ya Rs 12,000.

Mbali na michango hii hapohapo tena kuna utaratibu mwingine ni kuwa kama mtu anataka azikwe kwenye makaburi maalum ya makadiyyani ambayo huyaita "makaburi maalum ya peponi ya Rabwa"pindi atapofariki dunia italazimu kwamba badala ya ule mchango wa asilimia 6.25%[chanda Aam] atalipa asilimia 10% ya mali na atapeleka asilimia 10 ya mali yake kwa kiongozi wa Anjuman-e-Ahmadiyya na ataendelea kulipa asilimia 10%ya mapato yake yote huko mbele.

Masharti haya huanza kumbana tokea pale anapoazimia kuzikwa katika makaburi hayo sasa Kama mtu amekufa kisha maiti yake ikapelekwa Rabwah huku ikawa asilimia 10 ya mali yake bado haijapelekwa Kwa kiongozi wa jumuiya ya Ahmadiyya au Kama hajalipa michango mingine basi maiti yake huzuiwa kuzikwa hapo mpaka warithi wake wamalize kulipa michango hiyo vinginevyo maziko hayatafanyika kabisa. Kama mfuasi wa Ahamadiyya hatoi michango yote iliyotajwa hapa basi huwa si Ahamadiyya tena kama halipi chanda au kama anachelewesha malipo basi chanda hiyo itajilimbikiza akifa, itabidi ikusanywe kutoka kwa ndugu zake.

Yeyote yule mwenye madeni ya michango [chanda] jina lake litatangazwa hadharani na atachukuliwa kama muasi katika jumuiyya na mithili ya mnyama aliyekatwa mkia macho ya watu wote yatamwandama

Enyi rafiki wa jumuiyya!

Kwa maelezo yote haya nukta ninayotaka kuibainisha hapa ni jinsi jumuiya inavyochangamkia michango ya chanda na jinsi mitandao ulivyoratibiwa kwa kazi hii .je lakini mmepata kuona mkaguzi wa ZAKAT akija kutoka kituoni? Je zakat[ambayo ni faradh kwa kila muislamu] imewahi kukusanywa kwenu waahmadiyya?je ZAKAT imewahi kulimbikizwa katika madeni yenu?je mmeshawahi kusikia hotuba au waadhi unaousiana na zakat ukitolewa na Mirza Tahir mpaka anafariki? Je mmeshawahi kuona jitihadi yoyote ya uongozi wa kituo kuwahamasisheni kukusanya zaka? Bilashaka jibu litakuwa hapana je hamuoni hapa nguzo ya msingi ya uislamu imeachwa je uislamu unaweza kuwepo bila nguzo hiyo? ninachomaanisha hapa ni kuwa je Ahmadiyya bado tu inaweza kunasibishwa na uislamu bila nguzo hii?

Wapendwa Ahbab wa jumuiyya!

Mara nyingi mno mmesikia hotuba kadhaa wa kadhaa kutoka kinywani mwa "khalifa mirza Tahir [sasa ni hayati] juu ya ya baraka za jalsa salana dua njema kwa wanaohudhuria jalsa hii na dua nyingi zinatolewa kwa ajili yao. Mmewahi kusikia mawaidha na hotuba nyingi kuhusu jalsa salana zinazomshawishi mtu kuhudhuria. Tunasoma taarifa ndefu za jalsa salana, Rabwa na London katika majarida na magazeti ya jumuiya kama ‘Al Fazl’ ‘Khalid’ na Ansarullah. Kutokana na jitihada hizi,mtu ambaye amekuwa akisikia haya tokea utotoni pale afikiapo miaka 30-35 hupata imani kubwa na kila kipengele cha jalsa ambacho hakuna mtu asiye Ahamadiya anayeweza kujua hilo. Lakini je mmewahi kusikia hotuba juu ya hija kutoka kinywani mwa khalifa? Je Hazoor amewahi kuwaambia wanajumuiya juu ya Manasik-e-Hajj? Mmewahi kusikia waadhi juu ya hijja ukitolewa na kiongozi yoyote wa juu wa jumuiya? Jibu nikuwa hapana.kwa nini sasa iwe hivyo? Nguzo ya uislamu imevunjwa na badala yake mkazo unawekwa katika kuhudhuria jalsa salana je Hijja ngapi zilizofanywa na khalifa wa pili Mirza Bashirudin Mahmud? kwa umri wa miaka 51,akiwa imam wa Ahamadiya angeliweza kwenda hijja hata zaidi ya mara 30 lakini katika kuwalaghai watu alikwenda hijja moja tu!

Yeye ndiye aliyetakiwa awe mtu wa kushikamana zaidi na dini lakini angalia kafanya hijja ngapi? Yeye huyu ndiye aliyetangaza na kuwaambia waahmadiyya [makadiyyani] kwamba wale wote wasiokuwa wahamadiyya ni makafiri tena ni makafiri wa kutupa.

Waahmadiyya hawafanyi ibada ya Hijja kwa sababu ya vikwazo lakini wanatumia maelfu ya fedha [rupia] kwenda London kuhudhria jalsa salana muajiriwa wa serikali hawezi kuondoka nchini bila ruhusa maalum ya kiofisi lakini Ahamadiyya ambaye ni mtumishi wa serikali hufanya kila njia na kila aina ya ujanja kama kupata pasipoti za kughushi na kutoa maelezo ya urongo ili aende nje ya Nchi kuhudhuria Jalsa salana wanakwenda hata Qadiyyan kuhudhuria Jalsa salana kwa maneno mengine wanathibitisha kwa vitendo kuwa Jalsa ni muhimu kuliko Hijja.

Wapendwa Ahbab wa Jamaat!

Kama hivi sasa wewe unajiona muislamu unaona ni lazima na uamini nguzo tano za uislamu basi jiulize kichwani mwako hii jumuiya inakupeleka wapi kwa kitendo hiki cha kupuuzia na kuzikataa nguzo za uislamu [zaka na Hijja]? na kisha jiulize utawezaje hapo kuwa muislamu?

Wapendwa Ahbab wa Jumuiyya!

Nataka sasa muelezekeze akili zenu kwenye ili tatizo jingine la msingi.kinapofika kipindi cha uchaguzi wa kiongozi mkuu/Amir wa jumuiya za mitaa wakati wa kupiga kura wenye rekodi nzuri ya kutoa michango [chanda] ya miezi sita au zaidi bila kujali kama ni mcha mungu au ni mtu anayeheshimika au anasali sala tano bila kuwana rekodi nzuri za kutoa michango basi huenguliwa huwezi kupiga kura bila kujali kama ni mcha mungu au la na pia hawezi kushika madaraka ofisi.wanaopiga kura ni wale wasio na ucha mungu wowote na wasio swali kabisa lakini ni kwa kuwa tu wana sifa nzuri ya kutoa michango na pia kwa kuwa kabla ya uchaguzi mtu kulipa michango,jumuiyya inampa haki ya kuchagua Amir wa jumuiyya na viongozi wengine[wajumbe wa baraza kuu]si hivyo tu bali mtu huyo pia anayo haki kamili ya kuchaguliwa kama kiongozi na anaweza hata kuwa Amir wa jumuiyya.

Enyi rafiki zangu wa jumuiyya!

Hebu fikirieni! Jamani sifa pekee ya kuwa mpiga kura au kuwa kiongozi ni mchango tu [chanda] yaani pesa na sio uchamungu ni msiba mkubwa.yule anayelipa pesa basi ndio mchamungu na asiyelipa pesa anatupiliwa mbali.je huu sio utaratibu uleule wa kifisadi unaotumiwa na watu wa idara za serikali zinazonuka rushwa ambazo zimechafua mazingira ya ulimwengu?

Yule anayetoa pesa ndio hueshimiwa na kuwekwa mbele na yule asiyetoa pesa hudharauliwa.je Ahmadiya si inadai ni jumuiyya halisi ya kidini sasa vipi ukandamizaji huu wa tabaka la wenye nazo na masikini? Sasa ebu tutazame utaratibu wa uchaguzi wale wenye haki ya kupiga kura wote au baadhi yao ndio huwa viongozi mwanzoni kabisa mwa uchaguzi mtu mmoja husimama na kupendekeza yeyote yule kwa ajili ya nafasi yoyote ile.

Mtu ambaye jina limependekezwa yeye mwenyewe huwa hajui wala haombwi idhini yake na hata kama ridhaa yake atakataa kushiriki bado jina lake litakuwa miongoni mwamajina yaliyopendekezwa.

Halikadhalika mtu mwingine naye atasimama kumpendekezea mtu mwingine kwa ajili ya nafasi hiyohiyo kwa hiyo hawa wawili watakuwa ni wagombea wa nafasi moja hapo ndipo kura ya wazi hupigwa watu wataulizwa je wangapia wanaompendekelea yule wakwanza hapo hutakiwa kunyoosha mikono kama yule mgombea wa kwanza ni mtu mwenye mvuto basi kura zote humuangukia yeye na kama mgombea wa pili ana mvuto basi kura zote zitamsuburi yeye hakuna utaratibu wa kura za siri.

Ni dhahiri kuwa katika mikutano yote ya uchaguzi vijijini ni makabaila tu ni watu wa ovyo na wanapotoa kura kwa sababu tu wanauwezo na watu huogopa kumnyima kura kama huyo hali yakuwa yuko mbele yao akimuona kila mpiga kura.

Hivyo katika mikutano Kama hiyo pale mtu wa namna hiyo anapokuwa Amir au kiongozi ndio basi hubakia madarakani hadi kufa kwake kwani katika kipindi cha miaka mitatu uongozi wake hujiimarisha madarakani. Aidha jinsi utaratibu huo wa uchaguzi ulivyo ni kuwa mgombea haruhusiwi kuzungumza dhidi ya mpinzani wake hawezi hata kuzungumzia upande wake kwa wapiga kura. Hapo mtu fisadi huweza kuwa rais na kubakia kuwa hapo na atabaki katika nafasi hiyo kwani hakuna njia nyingine ya kumuondoa jumuiyya haiwezi kumuondoa kwani inasema wale waliomchagua ndio wanaweza kumuondoa je ni nani anaweza kumpigia kura ya kumkataa mtu na kujijengea uadui naye. Ni kutokana ana mfumo huo wa kizamanai usioleweka na uchaguzi ndio maana maamiri wengi wa jumuiya hukaa madarakani kwa muda mrefu kwa miaka na miaka.maamiri wa mijini na wilayani huweza kukaa madarakani kwa zaidi ya miaka ishirini sehemu nyingine hata miaka 30 kuna eneo Fulani mtu anashika madaraka kwa miaka 47. Maamiri wote hawa hukaa madarani hadi kufa kwao na kwa sababu hiyo wanakuwa juu ya kanuni na taratibu na sera wao hutawala mithili ya madikteta.ni kwa sababu hiyo ya sifa hizi za maamiri ndio maana watu huachana na jumuiyya ya Ahmadiyya. Hali hii inaendelea kila kukicha wengi miongoni mwa wale wanaoondoka katika jumuiyya ni wasomi na wamekinaishwa na utaratibu huu mbovu usio na misingi ya uadilifu.

Enyi Ahbaab wa jumuiyya!

Turudi tena kwenye huu utaratibu wa uchaguzi ninyi ndio mshamchagua mtu asiyekuwa muadilifu kuwa Amiri wa jumuiyya kama nilivyoelezea kwa kirefu kuwa kiongozi wa kijiji amekuwa Amir wa jumuiyya sasa maamiri hawa kutoka sehemu zote za hapa mfano Pakistan watachagua amir wa Pakistan au Amir wa jumuiyya nzima ‘khalifa’ hebu sasa chukulia kuwa ni jibini gani utapata hapa kutokana na maziwa yaliyotiwa sumu? Sasa ebu tukichambue kipengele hiki kabaila ndio kachaguliwa na kuwa Amir wa jumuiyya katika jumuiyya yake pia kuna Murabbi huyu murabbi amepata elimu ya dini miaka saba kabla ya kuteuliwa na kituo lakini kwa mujibu wa kanuni na taratibu za jumuiyya ni haki ya Amir kutoa hotuba ya ijumaa kwanza ikiwa anamuagiza "murabi’ basi ni murrabi pekee atakayetoa hotuba.

Sasa hotuba ya ijumaa ni wajibu wa kidini itakuwaje kwa Amiri wa jumuiyya kwa vile mtu kuwa Amir katika jumuiyya hakuna sharti la elimu ya dini na wala si lazima awe na elimu nyingine bali ukiwa mtoaji michango ndio sifa ya kuwa kiongozi wa jumuiyya yawezekana mtu akawa mbumbumbu ili mradi tu mtoaji michango basi ana haki ya kuwa Amir wa jumuiyya. Je mtu wa namna hii atakuwaje na uwezo kiutawala kwa hiyo Amir wa jumuiyya kwa namna zote na katika kila eneo liwe la utawala, kidini utungaji sera au jambo lingine lolote amir ndio ana uamuzi wa mwisho ni wake.hawajibishwi na mtu yeyote wala hawajibiki kwa mtu yeyote wala hawezi kupingwa popote kila shuri la kiutawala kila FATWA ya kidini itatoka kwake.

Enyi rafiki wa jumuiyya!

Sasa hebu tuone madaraka ya Amir aliyetajwa kama mfuasi wa kawaida wa Ahmadiyya anatofauti fulani ya maoni au uchungu dhidi ya uonevu, kauli, mwenendo na tabia ya Amir wa jumuiyya na tofauti juu ya jambo la kidini au utawala hapo Amir atapeleka malalamiko yake ngazi za juu hata kama upande wa amir ndio wenye kasoro,mfano tabia yake si njema kwa anaowaongoza lakini malalamiko ya huyo mnyonge yatatupwa na maneno ya Amir wa jumuiyya ndio yatazingatiwa hata kama hayuko katika haki na hata kama Amir akikusingizia jambo basi atasikilizwa na wewe utatengwa kutoka katika nidhamu ya jumuiyya au kufanyiwa manyanyaso Fulani.

Kwakuwa Amir sasa ndio ana ghadhabu na mfuasi huyu wa dhati wa jumuiyya aliyempinga basi na ‘khalifa’ wa jumuiyya duniani naye humkasirikia mfuasi huyo wa Ahmadiyya bila kuzingatia malalamiko yake kama ni haki au la kwa sababu tu eti Amir wa jumuiyya ni mwakilishi wake hivyo ni sharti khalifa naye akasirike na kwa mujibu wa imani za Ahmadiyya mungu humkasirikia pia mfuasi huyo na kama kweli mungu hukasirika hivyo ebu fikiri hatima yako! na kama atamfurahia mtu basi naye mungu humfurahia mtu huyo kwa maneno mengine ni kuwa mungu anawajibika kufuata matashi ya Amir wa jumuiyya kwa hiyo kama Amir wa jumuiyya akiruhusu atakapokuwa radhi naye Ahmadiyya huyo mwenye kutaka uadilifu.

Mfumo uliotajwa juu ndio haswa unatumika katika kazi za jumuiyya kwa hiyo basi picha inayojitokeza ni kuwa mungu anafuata matakwa ya wakandamizaji, mafisadi na wahalifu wa kila mji kwa yeyote ambaye yeye ataomba asamehewe basi mungu atamsamehe na yule ambaye yeye atapendekeza atiwe motoni basi mungu atamtia motoni kila mfuasi wa Ahamadiyya kimoyoni atakubaliana nami ni kweli tupu niliyotaja lakini hatokubali kamwe kukiri haya hadharani.

Wasalaam

Munawwar A..Malik Profesa wa fizikia Jhelun



Homepage